Sunday, July 26, 2009

Kikapu Afrika kutimua vumbi leo

Na Jacqueline Massano, Jijini
MASHINDANO ya mpira wa Kikapu ya Afrika Kanda ya tano yanatarajia kuanza kutimua vumbi leo hadi Agosti 2 mwaka huu nchini Uganda.

Katika mashindano hayo, Tanzania inatarajiwa kuwakilishwa na timu ya wanaume ya ABC na ya wanawake ya JKT.
Akizungumza na Alasiri, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu nchini,TBF, Lawrence Cheyo amesema timu hizo mbili zimepata tiketi za kushiriki kwenye mashindano hayo baada ya kushika nafasi za juu kwenye ligi ya taifa ya Tanzania.
Amesema mbali ya Tanzania, nchi nyingine zinazotarajia kushiriki kwenye mashindano hayo ni Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda, Ethiopia, Eritrea, Somalia na Sudan.
Cheyo amesema anaimani kuwa timu hizo zimefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya kwenda kushindana na kurudi na ushindi Tanzania.

No comments:

Post a Comment