Monday, July 13, 2009

Yanga kuita wake kesho


Na Daniel Mkate

WAKATI klabu ya soka ya Simba inaanza rasmi mazoezi leo kwa ajili ya Ligi Kuu Bara msimu huu, uongozi wa mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Yanga, umewaita wachezaji wake wote iliowasajili kuripori klabuni ifikapo kesho.Akizungumza na Alasiri mapema leo, mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya klabu hiyo, Emmanuel Mpangala, alisema wachezaji hao wameitwa kuripoti klabuni kwa ajili ya maandalizi ya ligi kuu."Tumeshawataarifu wachezaji wetu wote kuripoti klabuni ifikapo kesho, lakini muda wa kuingia kambini bado," alisema Mpangala.Mpangala alisema wachezaji hao wameitwa kwa ajili ya maandalizi ya ligi kuu inayotarajiwa kuanza Agosti 23 mwaka huu na kushirikisha timu 12.Hata hivyo, Yanga huenda ikatumia uwanja wake wa Kaunda kufanyia mazoezi pamoja na kuweka kambi kutokana na kukamilika kwa ukarabati wake wa mwaka mmoja na nusu.Mwenyekiti wa klabu hiyo, Iman Madega, awali alinukuliwa akisema timu yao itaweka kambi kwenye uwanja wake wa Kaunda baada ya kukamilika kwa asilimia kubwa ya ukarabati wake.Timu zitakazoshiriki ligi kuu pamoja na Yanga ni Simba, Manyema, Azam na African Lyon za Dar, JKT Ruvu ya Pwani, Mtibwa Sugar, Moro United za Morogoro, Prisons ya Mbeya, Majimaji ya Songea, Toto Afrika ya Mwanza na Kagera Sugar ya Kagera.

No comments:

Post a Comment