Sunday, July 19, 2009

50 Cent afuta tattoo


HOLLYWOOD, Marekani

CURTIS "50 Cent" Jackson ameamua kuondoa baadhi ya michoro maarufu ya mwilini mwake, ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kufanikiwa katika fani yake mpya ya uchezaji wa filamu Hollywood.
"Nimefuta baadhi ya tattoo kwasababu wakati wa kurekodi filamu, kama tunatakiwa kufika pale saa 12.00, mimi nalazimika kufika saa 2.00 usiku wa jana yake," 50 Cent alisema.
"Nalazimika kuwa na masaa manne kwa ajili ya kufanyiwa marembo ya kuficha michoro ya mwilini mwangu.
Hivyo nimeamua kufuta michoro ya mkononi. Mkono wangu wa kulia.
"Muasisi huyo wa lebo ya G-Unit hata hivyo hajamaliza michoro mingi aliyo nayo mwilini. Bado ana michoro mikubwa miwili mgongoni, iliyoandikwa "50 Cent" na tattoo inayosomeka "Southside".
Hatua hiyo ya 50 Cent inakuja kufuatia nyota huyo kucheza kama nyota wa filamu ijayo ya 'Streets Of Blood'.
Filamu hiyo ya drama, ambayo inawahusisha pia Sharon Stone, Val Kilmer na Michael Biehn, inazungumzia magangwe wa mitaani na rushwa kwa mamlaka za polisi baada ya janga la Kimbunga cha Katrina mjini New Orleans.
Nje ya Hollywood, single mpya ya 50 Cent ya "Ok, You're Right" kutoka katika albam yake mpya inayosubiriwa sana ya 'Before I Self Destruct', imeendelea kuchezwa kwa kasi na vitu vya radio.
Rapa huyo pia ameachia "mixtape" zake mpya za "War Angel" na "Forever King', aliyoitunuku kwa Mfalme wa Pop, Michael Jackson.

No comments:

Post a Comment