Sunday, July 19, 2009

Jada atamba 'kuduu' na Will Smith


NEW YORK, Marekani
KWA msanii yeyote, hakuna tuzo kubwa kama ya Oscar. Uwe katika orodha ya wanaowania tuzo, mshereheshaji au hata kuwepo pale ukumbini tu, kwasababu si rahisi kuona watu wakilikosa tukio hilo la kupita kwenye zulia jekundu.Na wakati hisia kwamba habari habari inayokuja ni ya ukumbini kwenye zulia jekundu, hilo waachie Will na Jada Pinkett-Smith wachague kilicho bora zaidi kwao. Kwa mujibu wa Jada, anachojali zaidi ni kutazamwa tu na Big Will kwa macho ya mvuto ili kuamsha 'mizuka' yake.“Ndani ya gari (limousine), tukiwa njiani kuelekea kwenye tuzo za Oscar mwaka huu, Will akaanza kuniangalia kwa jicho lile linalonifanya niwe chizi,” muigizaji huyo alisema kuliambia jarida la Shape. “Tukaanza kubusiana kimahaba, na kilichofuata...., unajua, wacha niseme tu kwamba tulikosa kuhudhuria kwenye zulia jekundu kwasababu vipodozi vyote nilivyojipamba vilikwisha.”Lakini kwa kuwa mambo hayo aliyafanya na mumewe Will, haizui mshangao. Hasa kama masimulizi hayo yametoka kwa mtu ambaye anayataja "mapenzi mengi" na mumewe kwenye magari, kwenye nyumba za rafiki zao, kwenye maduka ya mavazi na sehemu nyinginezo kama sehemu ya kudumisha ndoa yao na kuwafanya wasichokane.


No comments:

Post a Comment