Tuesday, July 14, 2009

Kabula kutoka na ushindi


Na Jacqueline Massano
Muimbaji wa muziki wa Injili nchini Kabula J. George anaratajia kuizindua albamu yake mpya aliyoipa jina la Ushindi yenye nyimbo nane ikiwa katima mfumo wa Tape, CD, VCD na DVD.Akizungumza na gazeti hili jana jijini Dar es Salaam, Mratibu wa uzinduzi huo George Kayala alisema kuwa, uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika Julai 5 mwaka huu katika ukumbi wa Matanta Msimbazi Center na maandali kwa ajili ya shughuli hiyo yanaendelea.Kayala alisema kuwa katika uzinduzi huo, kutakuwa na waimbaji wengi wakali wa muziki huo ambao kwa pamoja watakuwa na kazi ya kulihubiri Neno la Mungu kwa njia ya uimbaji.“Maandalizi yote kwa ajili ya uzinduzi wa Kabula yanaendelea, na siku hiyo kutakuwa na waimbaji mbalimbali ambao kwa pamoja watajumuika kulihubiri Neno la Mungu kwa njia ya uimbaji katika ukumbi huo,” alisema Kayala.Mratibu huyo alisema kuwa, nyimbo zote zilizomo katika albamu hiyo zinaupako wa ajabu kutokana na kuwagusa watu wengi ambapo wamekuwa wakizisikiliza na miongoni mwao wamekuwa wakipona magonjwa yao kwa njia ya kusikiliza vibao hivyo.

By Alasiri

No comments:

Post a Comment