Tuesday, July 14, 2009

Mauzo albamu za Jackson balaa

LONDON, England
ALBAMU za nyimbo za aliyekuwa bingwa wa midundo ya Pop Marekani, Michael Jackson zinazidi kushika chati za mauzo jijini London, nchini England, ambako mwanamuziki huyo alikuwa afanye onyesho lake la mwaka kabla ya kifo kumkuta.Albamu sita ziko kwenye chati za 10-bora, habari toka kwenye kampuni inayosimamia chati hizo za muziki ilisema jana.Albamu ya "The Essential", ndiyo inayoshika namba moja kwenye chati hizo.Bingwa huyo wa miondoko ya Pop, alifariki mwezi uliopita kutokana na kuugua ghafla ugonjwa wa moyo, ingawa bado kuna utata wa kifo chake.Nafasi ya tatu kwenye chati hizo, inashikiliwa na albamu yake ya "Off the Wall", ambayo wiki iliyopita ilikuwa katika nafasi ya 10, huku "Thriller", ikipanda mpaka nafasi ya sita.Albamu yake nyingine iliyomo kwenye 10-bora ni pamoja na "The Motown Years", iliyopigwa na Michael Jackson na kundi la Jackson Five, "Number Ones" na "Thriller 25". Wiki iliyopita, kampuni hiyo ilitangaza mauzo ya nakala 600,000 na hivyo kufanya nakala zilizouzwa tangu kufarika kwa Jackson kufikia milioni 1.5.

By Alasiri

No comments:

Post a Comment