Sunday, July 19, 2009

Kaseba, Cheka uso kwa uso Oktoba

Na Jacqueline Massano, DDC Mwenge

BONDIA wa kick Boxing, Japhet Kaseba amesema yupo kwenye mazoezi makali kwa ajili yakujiandaa na pambano dhidi ya Francis Cheka wa Morogoro inayotarajia kufanyika Oktoba 3 mwaka huu. Kwa mujibu wa Kasebe, pambano hilo linatarajia kufanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.Cheka kwa sasa anashikilia mkanda wa Tanzania wakati Kaseba ni bingwa wa Kick Boxing.Kaseba amesema baada ya kuona kuwa Cheka amekosa mpinzani amaeamua kuingia kambini kwa ajili ya kujifua ili aweze kupambana naye."Nimepumzika kwanza Kick Boxing, na sasa najifua ngumi ili niweze kupanda uliongoni na Cheka ambaye hadi sasa hana mpinzani," alisemaBondia huyo amewataka wapenzi na mashabiki wa ngumi kujitokeza kwa wingi siku hiyo uwanjani kwa ajili ya kushuhudia pambano hilo ambalo anadai litabeba hisia za watu wengi."Kila mmoja naimani ana hamu ya kumuona Cheka anapigwa baada ya kushinda pambano lake mara mbili dhidi ya Rashid Matumla, lakini kwa sasa naawambia kuwa hatoki," alitamba bondia huyo.

No comments:

Post a Comment