Monday, July 13, 2009

Simba mazoezini bila wageni

Simba
BAADA ya kukamilisha usajili wake, Simba imeanza mazoezi leo asubuhi ufukweni bila ya kuwa na wachezaji wake wa kigeni iliowasajili kwa msimu ujao wa Ligi Kuu ya Bara, na wala kocha wao Patrick Phir ambaye bado yuko mapumziko Zambia.
Akizungumza na Alasiri mapema asubuhi, kocha msaidizi wa Simba, Amri Saidi amesema timu hiyo imeanza mazoezi kwenye ufukwe wa Coco kwa ajili ya maandalizi ya ligi hiyo.
Wachezaji hao wa kigeni ambao hawajafika mazoezini ni Emmanuel Okwi wa Uganda, Owino Joseph, Hilary Echesa (Kenya) na Danny Mrwanda.
Amesema wachezaji wote waliosajiliwa na klabu hiyo wamehudhuria kwenye mazoezi hayo isipokuwa wale wa kigeni.
Amewataja baadhi ya wachezaji waliohudhuria mazoezini kuwa ni Juma Kaseja, Uhuru Suleiman, Amri Kiemba, Ramadhan Haruna, Salum Gilla, Ulimboka Mwakingwe, Deo Bonivanture 'Dida'.
Wengine ni Salum Kanoni, Mohammed Kijuso, Mussa Hassan 'Mgosi', Haruna Moshi, Mustapha Ally 'Bartez', Salum Kanoni, Naftari David, Juma Nyoso, Nico Nyagawa na Kelvin Yondan.
"Wa kigeni bado hajaripoti kwani wanaendelea kukamilisha taratibu fulani ila kuanzia kesho nahisi tunaweza kwa nao," alisema
Amesema programu hiyo ya ufukweni itakuwa ya wiki moja ambapo baadaye watahamia kwenye kambi ya Bamba Beach iliyopo Kigamboni.
"Hii ni kwa ajili ya kuwapa stamina wachezaji wetu, na itawasaidia sana," alisema
Amri amesema mazoezi hayo yatakuwa ya kwenda na kurudi kabla ya kuiweka timu kambini tayari kwa kuingia msituni.

No comments:

Post a Comment