Monday, July 13, 2009

Yanga yamsajili Bengo

WAKATI Simba ikiwa ina lengo la kumchukua kiungo wa klabu ya Villa ya Uganda, Stevin Bengo, watani zao wa Jadi, Yanga wamewazidi kete kwa kumchukua mchezaji huyo na kumfanyia majaribio.Yanga jana ilikuwa inawafanyia majaribio wachezaji wake wa kigeni kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.Habari zilizoifikia Alasiri jana uwanjani hapo, Simba ilikuwa na mpango wa kutaka kumsajili mchezaji huyo lakini ilishindikana baada ya kuzidiwa ujanja na Yanga ambayo iliizunguka.Inasemakana wakati kamati ya usajili ikiendelea kujipanga na kuhakikisha kuwa inamsajili mchezaji huyo, inakuja kutaamaki mchezaji huyo ameshaingia kwenye himaya ya Yanga.Hata hivyo, Alasiri ilipojaribu kuzungumza na mchezaji huyo alidai kwamba yeye alichofuata Tanzania ni kumalizana na uongozi wa Yanga na wala si vinginevyo."Mimi sijaja kwenye majaribio, nipo kwa ajili ya kujadiliana kitu na uongozi wa Yanga halafu naondoka narudi kwetu," alisemaMbali ya Bengo wachezaji wengine wenye nafasi kubwa ya kusajiliwa na Yanga, ni Mrwanda, Kamanzi Abdulkarim ambaye anachezea timu ya Alexander ya Ugiriki, na Kobongo Homole wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Mazoezi hayo yalionekana kuwa na msisimko baada ya mashabiki lukuki kujitokeza uwanjani hapo kwa ajili ya kuangalia vifaa hivyo vipya.Baadhi ya mashabiki waliokuwepo uwanjani hapo walisikika wakiwafagilia zaidi wachezaji kutoka Uganda, Rwanda na wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
======

No comments:

Post a Comment