Monday, July 27, 2009

TAFCA kuchaguana Agosti

Na Jacqueline Massano, Jijini

CHAMA cha makocha wa mpira wa miguu Wilaya ya Kinondoni, TAFCA, kinatarajia kufanya uchaguzi wake mkuu Agosti 9 mwaka huu.
Mwakilishi wa Chama hicho Kinondoni katika Mkutano mkuu wa TAFCA Taifa, Boniface Wambura amesema fomu za kuwania uongozi wa chama hicho zimeanza kutolewa jana.
Amesema fomu hizo zitakuwa zikipatikana katika ofisi za Chama cha Mpira wa Miguu Kinondoni, KIFA, na mwisho wa kuchukua na kurudisha umepangwa kuwa Agosti 3 mwaka huu.
Amezitaja nafasi zinazowaniwa kwenye uchaguzi huo kuwa ni ya mwenyekiti, makamu mwenyekiti, katibu mkuu, katibu msaidizi, mhazini, mhazini msaidizi, mjumbe wa mkutano mkuu wa TAFCA na wajumbe watatu wa Kamati ya Utendaji.
Amesema wanaowania nafasi za juu za mwenyekiti hadi mweka hazina msaidizi watatakiwa kuchukua fomu kwa sh.10,000 huku nafasi ya ujumbe watachukua kwa sh. 5,000.
Wambura amesema usajili kwa wagombea unatarajia kufanyika Agosti 5 mwaka huu na wanachama ambao hawajaripa ada zao wanatakiwa kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment