Wednesday, August 12, 2009

Ancelotti ashindwa kumnasa De Rossi



LONDON, England
CARLO Ancelotti ameshindwa kumfanya mchezaji aliyekuwemo katika kikosi cha Italia kilichotwaa Kombe la Dunia, Daniele De Rossi kuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa kumsajili katika klabu ya Chelsea.
Kocha huyo mpya wa Blues aliwasilisha dau la paundi milioni 22 kwa ajili ya kutaka kumsajili kiungo huyo wa Roma.
Lakini ofa yake ilitupiliwa mbali na klabu ya Roma inayoshiriki Serie A ambayo ilisisitiza De Rossi, 26, hauzwi kwa bei yoyote.
Mkurugenzi wa Roma, Bruno Conti alisema: "Pamoja na kiasi kilichotolewa kuwa kikubwa lakini kilikataliwa. Kwa Roma mchezaji huyu haguswi."Naye rais wa timu hiyo, Rosella Sensi aliongeza: "De Rossi hauzwi..."
Ancelotti kwa sasa ameandaa ofa ya paundi milioni 2.5 kwa ajili ya kiungo wa Norway, Erik Huseklepp, 24.
Nyota huyo amefunga mabao matano katika mechi zake sita za mwisho alizocheza na leo usiku anatarajia kuwemo katika kikosi cha timu ya taifa ya Norway itakapocheza na Scotland.Aston Villa na Newcastle nao pia wanamsaka mchezaji huyo.

No comments:

Post a Comment