Wednesday, August 12, 2009

Dida amgalagaza Kaseja mazoezini


Na Adam Fungamwango, Ubungo
TIMU ya Simba imeanza tena mazoezi yake kujiandaa na ligi kuu Tanzania Bara baada ya kumalizika kwa tamasha lao la Simba Day lililofanyika Agosti 8 na kufana.
Katika mazoezi hayo, Kocha Patrick Phiri alionekana kuwafua wachezaji wake katika eneo la kutafuta pumzi, baada ya kuwakimbiza kwa karibuni robo tatu ya mazoezi hayo.
Wachezaji wote wa Simba walikuwepo, lakini waliocheza mazoezi walikuwa 12 tu, huku wegine wakiwa pembeni kwa sababu mbalimbali.
Hata hivyo wachezaji ambao wanadaiwa kuwa ni majeruhi waliongozwa na Haruna Moshi, Jabir Aziz na Adam Kingwande hawakuwepo mazoezini hapo.
Wengine ambao hawakuwepo ni wale waliokwenda kwenye timu ya Taifa, Taifa Stars.
Katika mazoezi hayo, wachezaji waliotia fora katima kumkimbia ni Uhuru Selemani ambaye ndiye anayeonekena ana mbio kuliko mchezaji yoyote ndani ya Simba akimzidi hata Mussa Hassan Mgosi.
Kivutio kikubwa kilikuwa ni baina ya makipa wawili wa timu hiyo, Deogratius Munishi Dida na Juma Kaseja ambao katika pambano lao la mbio, Dida alimgaragaza Kaseja mara zote walizokuwa wakikimbia.
Dida alionekana ni mtaalam wa kukimbia kuliko Kaseja, ingawa naye mara kadhaa alikuwa akijitahidi kwa kila hali kumpita mwenzake, lakini ilikuwa ikishindikana na kuwa burudani ya aina yake kwenye uwanja wa Kinesi Bull, ambako timu hiyo inafanya mazoezi.
Wachezaji alioonekana jana ni Mgosi, Dida, Kaseja, Emmanuel Okwi, Joseph Owino, Hiraly Echessa, Amri Kihemba, Mohamed Kijuso, Mohamed Banka, Salum Kanoni, na Uhuru.

No comments:

Post a Comment