Tuesday, August 18, 2009

Arsernal kuifuata Celtic leo

GLASGOW, Scotland
ARSENAL leo itakuwa na kibarua cha kuwanyamazisha wapenzi wa soka wa hapa wakati itakapokabiliana na Celtic katika mchezo wa kwanza wa kusaka nafasi ya kucheza katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.
Celtic imekuwa tishio inapocheza kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Celtic Park na ina rekodi nzuri, ambapo iliilazimisha sare ya 1-1 Manchester United msimu uliopita.
"Siku zote hali ni tete Scotland," alisema kocha wa Arsenal, Arsene Wenger akizungumzia mchezo wa leo usiku."
Endapo tutacheza vizuri tunaweza kuifanya hali kuwa shwari..."
Celtic iliweka rekodi ya mahudhurio ya watazamaji kwa klabu za Ulaya wakati watazamaji 133,961 walipojitokeza kushuhudia kikosi cha Jock Stein kikiichapa Leeds katika nusu fainali ya mashindano ya Ulaya mwaka 1970 kwenye uwanja wa Hampden Park, lakini Wenger anaamini kuwa kikosi chake kitaendana na hali yoyote.
"Tumecheza Ulaya katika hali zenye ushindani mkubwa na kutokana na uzoefu wetu tunajua tufanye nini ili tuendane na hali, " aliongeza kocha huyo.

No comments:

Post a Comment