Monday, August 10, 2009

Majambazi yapora gari la mchezaji


LILLE, Ufaransa
MAJAMBAZI waliojifanya polisi walimfungia kwa muda katika buti la gari lake aina ya Mercedes Benzi mshambuliaji wa klabu ya Lille, Pierre-Alain Frau mapema jana, kabla ya kumuacha sehemu nyingine ya mji na kuchukua gari hilo.
Polisi walisema, wakati Frau akiingia katika gari lake, alikaribiwa na watu waliojitambulisha ni askari.
Mchezaji huyo alikuwa akirejea nyumbani baada ya kupata chakula cha jioni kufuatia Lille kupokea kipigo cha bao 2-1 na Lorient Jumapili.
Wavamizi hao walimlazimisha mchezaji huyo wa Ligue 1 kuingia ndani ya buti ya gari lake, na baadae waliliendesha gari hilo kutatisha mji.
Baadae majambazi hayo yalimtelekeza mchezaji huyo barabarani karibu na maeneo ya makazi ya watu kabla hawajaondoka na gari hilo la kifahari, kadi ya benki, simu ya mkononi na mamia ya pesa za euro.
Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi 10 kwa Frau kuporwa na majambazi.
Gari lake jingine liliporwa Oktoba mwaka jana.Klabu yake ilisema katika taarifa yake kuwa katika tukio hilo mchezaji huyo hakujeruhiwa na alifanya mazoezi pamoja na wenzake jana asubuhi.

No comments:

Post a Comment