Monday, August 10, 2009

Chelsea yampandia dau Ribery


LONDON, England
ROMAN Abramovich anatarajiwa kwenda Ujerumani kuwasilisha ombi la paundi milioni 40 kwa ajili ya kumsajili winga wa Bayern Munich, Franck Ribery.
Bilionea huyo mmiliki wa Chelsea ametaka kukutana na meneja mkuu wa Bayern Munich, Uli Hoeness.
Aliweka wazi nia yake ya kutaka kumsajili nyota huyo wa Ufaransa na yuko tayari kutoa kiasi kikubwa kabisa cha pesa ambacho hakuna klabu yoyote ya Uingereza iliyowahi kuahidi ili kumpata mchezaji huyo.
Chanzo kutoka ndani ya klabu ya Bayern kilisema: "Uli alishtushwa na simu aliyopigiwa na bwana Abramovich."
Bado tumedhamiria kumbakisha Ribery lakini Hoeness alikubali kukutana na Abramovich huko Ujerumani kuzungumzia ofa hiyo."
Mwezi uliopita, Manchester United na Chelsea zote zilionyesha nia ya kutaka kumsajili Ribery katika kipindi hiki cha majira ya joto.
Hatahivyo, Man United bado haijawasilisha ofa, na Abramovich anaonekana kutaka kuizidi kete kwa kuharakisha kuwasilisha ofa hiyo.
Kocha mpya wa Blues, Carlo Ancelotti aliahidiwa na bilionea huyo wa Russia kusaini majina makubwa lakini hadi sasa maombi yake ya kutaka kumsajili Kaka na Alexandre Pato yameshindwa kufanikiwa.
Naye Ribery tayari alishaweka wazi kuwa anataka kujiunga na Real Madrid.Munich inahofu huenda Ribery akawa amesaini mkataba awali kama ule wa Cristiano Ronaldo ambao utamwezesha mchezaji huyo kuondoka katika timu hiyo na kutua Real Madrid majira yajayo ya joto.
Hasira za Munich dhidi ya jeuri ya Real Madrid, klabu hiyo ya Ujerumani huenda ikaamua kumuuza mchezaji huyo kwa Chelsea.

No comments:

Post a Comment