Wednesday, October 28, 2009

Benitez amnyemelea Mata

London, England
RAFA Benitez yuko tayari kumsajili wingi wa kimataifa wa Valencia Juan Mata wakati wa usajili mdogo Januari mwakani..Mata, 21, amekuwa na wakati mgumu msimu huu, na Valencia wanaonekana kuwa tayari kumuuza kutokana na kukabiliwa na ukata.Huenda wakampiga bei kwa paundi za kiingereza milioni 16.Benitez ana uhakika kumnasa mchezaji huyo ambaye mkataba wake unamalizika mwaka 2012 kwa mshahara wa paundi 10,000 kwa mwenzi.Baba mzazi wa Mata, Juan Snr, ambaye pia ni agenti alisema: "Tunataka Valencia watambue kipaji cha kweli cha mtoto, na sio suala la pesa tu."Juan aliongeza: "Suala hili litamalizwa na klabu na wakala. Benitez ni kocha mkubwa, nataka kuweka mkazo kwenye soka bila usumbufu."

No comments:

Post a Comment