Wednesday, October 28, 2009

Kaduguda amkimbia Mwalusako

Na Jimmy Charles
KATIBU Mkuu wa Simba Mwina Kaduguda jana alimkimbia Katibu Mkuu wa klabu ya Yanga Lawrence Mwalusako katika mahojiano maalum juu ya mchezo wao wa keshokutwa yaliyoandaliwa na Radio One katika kipindi chake cha kumepambazuka michezo.
Kaduguda, Mwalusako na Afisa Habari wa Shirikisho la soka nchini (TFF),Frolian Kaijage walialikwa kwa pamoja kwenye kipindi hicho kwa ajili ya kuujadili mchezo huo wa Jumamosi, utakaochezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo ni Mwalusako na Kaijage pekee ndio waliofika kwenye kipindi hicho kilichokuwa kikiongozwa na Maulidi Kitenge, ambapo Kaduguda alishindwa kuungana na wenzake.
Akizungumzia kitendo cha Katibu huyo wa Simba kuingia mitini Kitenge alieleza kuwa Kaduguda alipewa taarifa za kufika kwenye kipindi hiocho mapema lakini hawakujua nini kilimsibu hadi kushindwa kufika.
"Kaduguda ameshindwa kutokea ingawa alipewa taarifa za kushiriki kwenye kipindi hicho mapema,"alisema Kitenge.

No comments:

Post a Comment