Saturday, October 31, 2009

Puyol aongeza mkataba Barca


MADRID, Hispania
NAHODHA wa Barcelona, Carles Puyol ameongeza mkataba mwingine tena wa miaka mitatu na mabingwa hao wa Barani Ulaya ambao unatarajia kumalizika Juni, 2013, klabu hiyo ilisema jana.
Dili hilo la beki huyo wa Hispania mwenye miaka 31, limegharimu dola milioni 14.8 za kimarekani, ambapo mkataba huo pia unatakiwa kumuwezesha kucheza asilimia 60 za mechi zote za klabu hiyo kwa msimu, Barcelona ilisema kupitia tovuti yake ya mawasiliano.
"Nina furaha na ninajiamini na klabu, benchi la ufundi na wachezaji wenzangu kwa kile walichonionyesha," Puyol aliiambia TV ya Barca

No comments:

Post a Comment