Saturday, October 31, 2009

Kizungu champiga chenga Teves

London, England

CARLOS Tevez ameshauriwa kujifunza lugha ya kiingereza.
Mara nyingi Tevez, amekuwa akihitaji mkalimani kwa ajili ya kumsaidia kupokea maelezo pamoja na kuwepo England kwa miaka mitatu.
Lakini mwenzake kutoka Argentina, Pablo Zabaleta anaongea kiingereza kizuri katika kipindi cha miezi 12 tu England.
Na amemuambia Tevez wakati umefika wa kujifunza kiingereza.
Zabaleta, 24, alisema: "Ni muhimu. Najifunza kiingereza mara moja kwa wiki, na 'kizungu' kinaonyesha mafanikio sasa. najaribu, na kujaribu.
"Sikuwa naongea kiingereza kabla ya kuja, lakini kupitia masomo sasa naweza kuongea.
"Nimemwambia Carlos anaweza kuja kwangu ili nimfundishe."Wakati fulani anajaribu kuongea, lakini ni lazima kujifunza kwa sababu tunahitaji kuongea na wachezaji wenzetu na makocha.
"Na hasa ukizingatia kwa sasa tunaishi England."
'Kizungu' cha Zabaleta kinatia moyo hasa kwa mtu ambaye hakuweza hata kuongea neno alipojiunga na Man City akitoka Espanyol Agosti 2008.
Tevez, hajawahi hata siku moja kufanya mahojiano kwa kiingereza.Watu wengi wakiwemo waandishi wa habari walishangaa kuona mchezaji huyo akizungumza Kihispania wakati akitangaza kujiunga na City kutoka Man United pamoja na kukaa misimu miwili England.

No comments:

Post a Comment