Saturday, October 31, 2009

Ronaldo amuita Rooney Real Madrid

(Wayne Rooney)
(Cristiano Ronaldo)
London, England
CRISTIANO Ronaldo amemshauri Wayne Rooney kumfuata Real Madrid. Mshambuliaji huyo wa bei mbaya, anasema Real inaweza kutisha zaidi iwapo itakuwa na nyota huyo wa Manchester United.
Ronaldo aliambia SunSport: "Wayne atafanya vizuri hapa. Nadhani anaweza kuwa msaada mkubwa kwetu.
"Itakuwa vizuri zaidi kama atakuja. Hii ni sehemu nzuri kwa wachezaji wa viwango vya juu duniani."Wayne ana ila kitu kinachoweza kumfanya kuwepo hapa.
"Ameweza kuonyesha waziwazi ni kwa kiasi gani amekuwa tishio England kwa miaka ya hivi karibuni.
"Na hakuna shaka kwamba hata akija hapa ataendelea kuwa juu. Itakuwa furaha kumuona siku moja hapa Real Madrid.
"Najua inaweza kuwa ngumu kwake kuja England."Anaipenda sana England, anaipenda Manchester, na isitoshe yeye ni kijana wa Liverpool Na United ni klabu nzuri kwake.
Lakini huwezi kujua nini kitatokea baadaye.
Ndoto ya Ronaldo kucheza Real imekumbana na matatizo baada ya kuumia kifundo cha mguu, huku timu yake ikipoteza mechi tatu kati ya tano ilizocheza.
Moja ya kipigo kibaya ni kile cha wiki hii cha mabao 4-0 dhidi ya timu ya daraja la tatu Alcorcon, ambapo kimemuweka pabaya kocha Manuel Pellegrini.

No comments:

Post a Comment