Thursday, October 29, 2009

Rais amtetea kocha wa Real Madrid

(Manuel Pellegrini-Kocha wa Real Madrid)
(Florentino Perez-Rais wa Real Madrid)
MADRID, Hispania
KOCHA wa Real Madrid Manuel Pellegrini anahitaji "muda na utulivu" ili kukamilisha kibarua cha kukisuka kikosi chake ghali kuwa timu kamili, kwa mujibu wa rais wa klabu hiyo Florentino Perez.
Real Madrid bado inawewesekana kutokana na kipigo cha bao 4-0 ilichokipata Jumanne timu ya daraja la tatu ya Alcorcon katika mchezo wa kwanza wa Kombe la Mfalme, na kuzua wasiwasi kkwa vyombo vya habari kuhusu hatma ya kocha huyo kabla ya mchezo wao wa Jumamosi wa La Liga dhidi ya Getafe.
"Napenda kupeleka ujumbe wa kuwatuliza wapenzi, "alisema Perez, aliyetumia euro milioni 250 (sawa na dola za Marekani milioni 369) kwa kununulia wachezaji kama akina Cristiano Ronaldo na Kaka katika kipindi kilichopita cha usajili.
"Inatakiwa kukumbuka kuwa wachezaji wengine wageni waliwasili kabla ya kuanza kwa msimu wa ligi na hii inahitaji kipindi fulani cha kuzoea mazingira."
"Msimu huu ndio kwanza una miezi miwili na bado tunajaribu kuunda timu."
Tiny Alcorcon, aliyecheza katika ligi hiyo akiwa katika kikosi cha vijana cha Real Madrid na bajeti ya timu hiyo ilikuwa ndogo zaidi ya mara 400 zaidi ya vigogo hao wa Hispania, aliweza kukisambaratisha kikosi cha kocha Pellegrini licha ya kuwepo kwa mabeki wa Hispania Raul Albiol na Alvaro Arbeloa, na wachezaji wengine wa kimataifa.
Kipigo hicho kilifuatia suluhu ya wiki iliyopita huko Sporting Gijon katika La liga na kuruhusu mabingwa Barcelona kuongoza ligi hiyo kwa pointi tatu zaidi kileleni na kipigo cha 3-2 nyumbani dhidi ya Milan katika Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.

No comments:

Post a Comment