Monday, November 30, 2009

KIPA MPYA YANGA KUJARIBIWA LEO

WAKATI ikiendelea na mazoezi kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, kipa mpya wa Yanga kutoka Ghana, Yaw Berka anatarajiwa kufanyiwa majaribio leo uwanjani hapo.
Berka ambaye aliwahi kuichezea timu ya tifa ya vijana ya Ghana, atafanyiwa majaribio akiwa chini ya kocha mkuu wa timu hiyo, Kostadin Papic.
Yanga kwa sasa ipo kwenye mchakato wa kusajili wachezaji katika dirisha dogo la usajili ambalo linafikia tamati leo.

No comments:

Post a Comment