Wednesday, November 11, 2009

Ronaldo kuikosa Ureno

OBIDOS, Ureno

Cristiano Ronaldo, winga wa Ureno atakosa mechi mbili za kusaka nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Bosnia, lilisema Shirikisho la Soka la Ureno (FPF), katika taarifa yake jana.
Ronaldo hajapona maumivu yake ya kifundo cha mguu, na hatacheza mchezo utakaofanyika Lisbon Jumamosi na ule wa Zenica siku nne baadaye.
"Baada ya uchunguzi, imekubaliwa kuwa mchezaji huyo bado hajafikia kigezo vya kiafya kujiunga na timu ya taifa ya Ureno, "ilisema FPF.
Mchezaji huyo wa Real Madrid aliyesajiliwa kwa ada ambayo ni rekodi duniani, aliumia mwishoni mwa Septemba wakati Ureno ikishinda 3-0 dhidi ya Hungary na tangu wakati huo hajawahi kucheza.

No comments:

Post a Comment