Friday, November 27, 2009

Sissoko akerwa na Ubaguzi wa rangi

MILAN, Italia
KIUNGO wa Juventus, Mohamed Sissoko amezitaka mamlaka zinazosimamia mchezo wa soka kuchukua hatua kali zaidi baada ya mashabiki wa klabu hiyo kuonyesha vitendo vya ubaguzi wa rangi.
Juve ililazimika kucheza bila watazamaji wake msimu uliopita kufuatia mashabiki wake kuimba nyimbo za ubaguzi wa rangi wakimlenga mchezaji wa Inter Milan, Mario Balotelli waliposema, 'hakuna mtaliano mweusi'.
Klabu hiyo ilitozwa faini kufuatia kuendelea kutoa maneno ya kibaguzi dhidi ya mchezaji huyo mwenye asili ya Afrika kwenye mechi ya Jumapili waliyoshinda bao 1-0.
Hata hivyo, vitendo hivyo vilishuhudiwa tena kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa waliyofungwa bao 1-0 dhidi ya Bordeaux Jumatano wiki hii
Sisi kama wachezaji tunapinga vitendo hivi," alisema Sissoko mchezaji wa kimataifa wa Mali wakati akiongea na Radio ya Italia Alhamisi."
Juventus imechukua hatua zote kuhakikisha vitendo hivi havitokei tena, lakini ni jukumu la mamlaka zingine kuingilia kati.
"Shirikisho la Soka Ulaya-UEFA litafanya uchunguzi kuhusu madai hayo ambayo yanaweza yasiwe na nguvu kwa vile yalitokea kabla ya kuanza kwa mchezo hivyo kutokuwepo kwenye ripoti ya mwamuzi.
Juventus wanaoshika nafasi ya pili kwenye msimamo, wanatarajia kupambana na vinara wa ligi hiyo Inter Milan Dec. 5, na kocha Jose Mourinho amesema ingekuwa jambo zuri kama mchezo huo ungehamishwa toka Turin.

No comments:

Post a Comment