Friday, November 27, 2009

Grant kocha mpya Portsmouth

LONDON, England
Avram Grant ametangazwa kuwa kocha mkuu wa timu ya Portsmouth akichkua nafasi ya kocha Paul Hart aliyetimuliwa mwanzoni mwa wiki hii, taarifa ya klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya England ilisema jana.
"Avram ni kocha mwenye uzoefu na anaheshimika kwa kiwango chake cha juu ufundishaji. Bodi ya wakurugenzi inaamini kuwa ataisaidia klabu kuepuka kushuka daraja," alisema mwenyekiti mtendaji Peter Storrie kupitia tovuti ya klabu hiyo.
Grant atakuwa kwenye benchi la timu hiyo Jumamosi wiki hii wakati atakapopambana na Manchester United.
"Anaijua klabu, wachezaji na mfumo mzima hapa Fratton Park, hivyo ni sahihi kumtangaza kuwa kocha," alisema Storrie.

No comments:

Post a Comment