Monday, November 30, 2009

UCHAGUZI SIMBA MWAKANI

WAKATI wanachama wa klabu ya Simba wakilicharukia Shirikisho la Soka nchini, TFF, kuwa limekwamisha kufanyika kwa uchaguzi mkuu, uongozi wa klabu hiyo umetangaza uchaguzi huo sasa utafanyika Januari 17, mwakani.
Kikao cha kamati ya utendaji ya klabu hiyo iliyokutana usiku wa kuamkia leo, umeamua kwa kauli moja kuwa uchaguzi huo utafanyika Januari mwakani na wala si Desemba mwaka huu kama ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi.
Kwa mujibu wa taarifa toka kwa mmoja wa viongozi wa klabu hiyo ni kwamba kikao hicho kimeamua uchaguzi huo kufanyika tarehe hiyo ili kupisha zoezi la ugawaji wa kadi, kikao cha mapato na matumuzi na mkutano mkuu.

No comments:

Post a Comment