
Mshambuliaji wa Sweden Zlatan Ibrahimovic alifunga bao pekee lililoitoa Barcelona kifua mbele baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Real Madrid nyumbani na kurejea kileleni mwa msimamo wa Primera Liga.\Mchezaji huyo alifunga bao hilo katika dakika ya 56 na Barca ilijikuta ikipata pigo baada ya mchezaji wake Sergio Busquets kutolewa nje kwa kadi nyekundu muda mfupi baada ya bao hilo, lililoiwezesha timu hiyo kuwa pointi mbili zaidi kileleni dhidi ya wapinzani wake hao wakubwa ikiwa na pointi 30 baada ya kucheza mechi 12.
No comments:
Post a Comment