Monday, November 16, 2009

Yanga uso kwa uso na Maafande wa Prison


MABINGWA wa soka wa Ligi ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga, leo wanatarajia kumaliza mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo kwa kumenyana na Prisons ya Mbeya kwenye mechi itakayochezwa uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Katika mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya vuta ni kuvute, Yanga inaingia uwanjani ikiwa katika nafasi ya nne na pointi 18 huku Prisons ikiwa pointi nane ikiwa nafasi ya 10.
Ili ziweze kufanikiwa kupanda katika msimamo wa ligi, timu hizo mbili zote kwa pamoja zitaingia uwanjani huku zikiwa na hamu ya kufanikiwa kuibuka na pointi tatu ili ziweze kupiga hatua mbele.
Ikiwa Yanga itafanikiwa kushinda katika mchezo huo, moja kwa moja itapanda hadi nafasi ya tatu huku ikiiacha Mtibwa Sugar katika nafasi ya nne.

No comments:

Post a Comment