Monday, December 28, 2009

Hali ilivyokuwa fainali Kombe la Tusker

Athuman Idd 'Chuji' akimzuia mchezaji wa Sofapaka wakati wa fainali za Kombe la Tusker zilizofanyika jana. Katika mchezo huo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 na kuchukua kombe hilo.
Kipa wa timu ya Sofapaka, Wilson Obungu akiwapigia kelele wachezaji wenzake wakati wa mechi ya fainali hizo.


Mshambuliaji wa pembeni wa Yanga, Mrisho Ngassa akiwatoka wachezaji wa Sofapaka.
Baadhi ya wachezaji wa Yanga, wakiwa wamembeba kocha wao, Kostadin Papic mara baada ya kuchukua ubingwa jana.
Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete akionyesha kikombe juu baada ya kuzawadia alipoibuka kuwa mfungaji bora kwenye michuano hiyo. Pia mchezaji huyo alipewa dola 2,000.

Katibu mkuu wa Simba, Mwina Kaduguda akipokea mfano hundi ya sh. milioni 10 baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa tatu wa michuano hiyo.

Baadhi ya wachezaji wa Yanga, wakiwa na mwenyekiti wao Iman Madega wakishangilia baada ya kupewa kombe la Tusker.

Nahodha wa Yanga, Abdi Kassim 'Babi' na kocha mkuu wa timu hiyo, Papic akionyesha juu mfano wa hundi ya sh. milioni 40 baada ya kuibuka mabingwa wa michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment