Wednesday, December 23, 2009

Yanga kuingia mafichoni

KIKOSI cha wachezaji 26 wa mabingwa wa soka nchini, Yanga kinatarajia kuingia mafichoni jioni ya leo kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya kesho dhidi ya watani wao wa Jadi, Simba.
Mechi hiyo ya nusu fainali ya pili ya michuano ya Kombe la Tusker inatarajia kufanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hata hivyo, inasemekana kuwa huenda Yanga ikamkosa mchezaji wake mmoja Stevin Bengo wa Uganda, ambaye yuko kwao kutokana na kuumwa.

No comments:

Post a Comment