Thursday, October 29, 2009

Jahazi kumtoa Daktari wa Mapenzi leo

Na Mwandishi Wetu

KUNDI la Jahazi Modern Taarab `Wana Nakshi Nakshi' leo litazindua albamu yake ya Daktari wa Mapenzi, katika onyesho litakalofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa kundi hilo, Mfalme Mzee Yussuf alisema onyesho hilo litakuwa na aina yake na litapambwa na burudani kibao.
Pia, inaelezzwa kuwa uzinduzi huo utakwenda sambamba na sherehe za kundi hilo za kutimiza miaka mitatu tangu kundi hilo liliposajiliwa rasmi na kuanza kutoa burudani katika kumbi mbalimbali.
"Uzinduzi wetu wa Oktoba 30 (leo) utakwenda sambamba na birthday yetu ya kutimiza miaka mitatu tangu kundi liliposajiliwa rasmi, litakuwa onyesho kubwa sana na la aina yake, ambapo pia kutakuwa na wasanii wengine watakaopamba.
Mbali na Daktari ya Mapenzi inayobeba jina la albamu, vibao vingine vilivyomo katika albamu hiyo ni 'Chokochoko', 'Domo Kaya', 'Fungu la Mungu Sikosi' na 'Roho Mbaya Haijengi'.
Tayari nyimbo za albamu hiyo mpya zimesharekodiwa na zimeanza usikika katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini na zimeonyesha kupendwa sana.Tayari kundi hilo linatamba na albamu zake nne ambazo ni Two In One, Kazi ya Mungu, Tupendane na VIP, ambayo inaendelea kutesa hadi sasa kwa makali yake.
Kibao cha Daktari wa Mapenzi kilipigwa kwa mara ya kwanza Idd Mosi katika ukumbi wa Travertine na kuwachengua vilivyo wapenzi hasa kibwagizo chake kisemacho "Baridi, baridi imenishika..." na kuwafanya wapenzi kuwehuka.

No comments:

Post a Comment