Wednesday, November 18, 2009

Algeria, Misri uso kwa uso leo

KHARTOUM, Sudan
Wachezaji wa Algeria, wamesema wako fiti kwa asimilia 100 kukabilina na Misri mjini Khartoum, Sudan katika mechi muhimu ya kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia, 2010-Afrika Kusini.
Baada ya mechi ya Jumamosi kujawa na vurugu, maelfu ya mashabiki kutoka Algeria na Misri wamewasili mjini Khartoum kushuhudia mechi hiyo, ambapo katika hali ya kuimarisha ulinzi, askari 15,000 watakafanya kazi hiyo.
"Timu yote iko kamili kwa ajili ya vita hii," alisema mlinzi wa Algeria, Madjid Bougherra anayecheza soka ya kulipwa na klabu ya Rangers.
"Kila mchezaji yuko fiti." Alisema, mlinzi anayecheza timu ya VfL Bochum, Antar Yahia, atacheza mechi ya leo baada ya kupata nafuu.
Kocha wa Misri Hassan Shehata, ambaye bado ana imani na kikosi chake kufuzu kufuatia kuibuka na ushindi kwenye mechi ya kwanza, huku bao la ushindi likifungwa kwa kichwa na Emad Moteab dakika tano kabla ya kumalizika mchezo, amesema atatumia mbinu nyingine ili kupata ushindi

No comments:

Post a Comment