Friday, November 13, 2009

Barasa aikimbia Simba, Yanga

Jacqueline Massano

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Yanga, amendoka leo kurejea kwako, Nairobi nchini Kenya na kuziacha kwenye mataa klabu za Simba na Yanga.
"Nimeamua kuondoka kurudi nyumbani (Kenya) baada ya kuona hakuna la maana walilosema viongozi wa Yanga," alisema mchezaji huyo wakati akiongea na Alasiri mapema leo.
"Naona haipo sababu ya kuendelea kukaa hapa (Tanzania) bila kuwa na kazi ya kufanya, nimeamua kurudi nyumbani. Mwenye shida na mimi, nadhani atalazimika kwanza kunitafuta toka Kenya," aliongeza zaidi.
"Navyozungumza na wewe napanga mizigo yangu ili niondoke, mambo yakienda vizuri usiku nitakuwa Nairobi," alisema zaidi mshambuliaji huyo ambaye kwa wiki nzima amekuwa gumzo kwenye vyombo mbalimbali vya habari.
Kulikuwa na taarifa kwamba, nyota huyo wa Kenya amekuwa akiwakwepa viongozi wa Yanga, lakini mwenyewe alipoulizwa hilo alisema: "Kuna maneno ya mitaani, ndio kama hayo unayoniuliza. Kwanini niwakwepe?. Eti nataka kukimbia, kwenda wapi, na ili iweje?"
"Niko tayari kurejea tena, kama kuna timu inanihitaji---Simba au Yanga, zinanihitaji ni suala la makubaliano tu," alisema zaidi.
Aidha, Barasa amesema amefanya mazungumzo na viongizi wa Simba lakini hawajafikia makubaliano na taarifa kwamba amesaini mkataba hazina ukweli.

No comments:

Post a Comment