Monday, November 23, 2009

Beckham anogewa na soka

LONDON, England
David Beckham amesema ataendelea kucheza soka England hata baada ya kumalizika kwa fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Afrika Kusini.
"Kama tutashinda Kombe la Dunia na kufikia rekodi, litakuwa jambo zuri kumaliza, lakini bado naona ni ngumu kuacha kucheza," alisema kiungo huyo wa L.A. Galaxy ya Marekani.
"Hata kama ndoto yangu itakuwa ya kweli, bado nitaendelea kucheza kwenye nchi yangu. Ningependa niendelea kushiriki kwa njia moja ama nyingine."
Hamu yangu kwa timu na nchi ni kubwa, na hii haitabadilika," aliongeza Beckham ambaye atafikia rekodi sawa na kipa wa Englansd Peter Shilton ya mechi 125 kama atacheza mara kwa mara kwenye fainali za mwakani.

No comments:

Post a Comment