Monday, November 23, 2009

Laazizi wa Britney jela siku 45

LOS ANGELES, Marekani
MPIGA picha aliyewahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi kwa muda mfupi na msanii Britney Spears, amehukumiwa kwenda jela siku 45 baada ya kupatikana na hatia ya kukwaruzana na afisa mmoja wa polisi.
Adnan Ghalib, 37, aliyekuwa karibu na mrembo huyo msanii wa muziki mwaka 2007, mbali na kifungo hicho pia ametakiwa kushiriki katika mafunzo ya kuzuia na kudhibiti hasira.
Mwendesha mashitaka wa Los Angeles, alisema Februari mwaka huu, Ghalib alikiuka agizo la mahakama lililomtaka kuwa mbali na Spear na familia yake, na aliposimamishwa na afisa huyo alianza kukwaruzana naye.
Mwenyewe Ghalib alikiri shitaka hilo, lakini kosa lingine alilofunguliwa kutokana na tukio hilo lilifutwa.
Spears, 27, alianza mahusiano ya kimapenzi na Ghalib Desemba 2007 wakati huo msanii huyo akiwa kwenye wakati mgumu kufuatia mtafaruku uliopelekea kupewa talaka na aliyekuwa mme wake.

No comments:

Post a Comment