Thursday, November 12, 2009

Dunga aimalisha kikosi cha 'kuiua' England

SAO PAULO, Brazil
KOCHA Dunga amemuita kwenye kikosi cha Brazil mlinzi wa AC Milan, Thiago Silva kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya England wiki ijayo.
Silva anajiunga na kikosi hicho kuchukua nafasi ya mlinzi wa Benfica, Luisao kufanyiwa upasuaji mdogo wa kidole cha tumbo.
Milan imekubali ombi la kufuatia muda wa kuruhusu wachezaji kufika, lakini ikifanya hivyo pia kwa lengo la kujenga mahusiano mazuri na Shirikisho la Soka Brazil, kwa mujibu wa taarifa zilizotumwa kwenye tovuti ya klabu hiyo jana.
Luisao alifanyiwa upasuaji jana, na kuamua kujiondoa kwenye kikosi cha Brazil kwa ajili ya mechi dhidi ya England itakayochezwa mjini Doha.

No comments:

Post a Comment