Tuesday, November 24, 2009

FIFA kujadili bao la mkono la Henry

LONDON, England

SHIRIKISHO la Kimataifa la Soka Ulimwenguni-FIFA, linatarajia kufanya mkutano mwezi ujao, ambapo pamoja na mambo mengine litajadili tukio la kuucheza mpira kwa mkono lililofanywa na nahodha wa Ufaransa, Thierry Henry kwenye mechi ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Lakini pia chombo hicho kikubwa chenye dhamana ya kusimamia mchezo wa soka, kitajadili vurugu zilizotokea kwenye mechi kati ya majirani wawili, Misri na Algeria wiki iliyopita.
FIFA mpaka sasa imekataa kuchukua hatua zozote dhidi ya Henry anayetuhumiwa kuucheza mpira kwa mkono na kupelekea bao la kusawazisha kwa Ufaransa wakati ikicheza na Ireland.
Chama cha soka cha Ireland kiliomba mechi hiyo kurudiwa, hata hivyo ombi lao halikukubaliwa.

No comments:

Post a Comment