Tuesday, November 24, 2009

Vigogo vya Soka Ulaya dimbani leo

Ni Liverpool, Barca, Bayern
LONDON, England

Vigogo Barcelona, Liverpool na Bayern Munich leo zenye rekodi ya kutwaa ubingwa wa vilabu barani Ulaya, ziko katika hatari ya kutolewa katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya leo na kesho.
Mabingwa watetezi Barcelona watakabiliana na mshambuliaji wao wa zamani Samuel Eto'o katika pambano lao dhidi ya Inter Milan na endapo itafungwa, huku timu ya Russia ya Rubin Kazan itaibuka na ushindi dhidi ya Dynamo Kiev, itakuwa imefungasha virago katika mashindano hayo.
Liverpool nayo leo iko katika hatari ya kutupwa nje kwa vile hata kama itashinda, bado kuendelea kwake mbele kwenye michuano hiyo kutategemeana matokeo ya timu zingine, endapo Fiorentina itaifunga Olympique Lyon ambayo tayari imeshafuzu, basi safari ya Liverpool itakuwa imeiva.
Miamba mingine ya Ujerumani, Bayern Munich ambayo itakuwa nyumbani ikicheza dhidi ya Maccabi Haifa ikijua kuwa, hata wakishinda kama wanavyotarajiwa watatupwa nje endapo Juventus itaifunga Girondins Bordeaux ambayo tayari imeshafuzu katika hatua ya timu 16 bora.
Katika mechi zingine, Arsenal itaungana na Lyon, Bordeaux, Chelsea, Porto, Manchester United na Sevilla katika hatua hiyo ya mtoano inayoshirikisha jumla ya timu 16 wakati AC Milan na Real Madrid pia zina nafasi nzuri ya kusonga mbele katika mashindano hayo.
Inter itakuwa mgeni wa Barcelona katika mchezo wa Kundi F utakaofanyika leo, ambao unakodolewa macho na wengi.
Waitalia wanaoongoza kundi hilo baada ya kuifunga Dynamo Kiev katika mchezo wa mwisho wiki mbili zilizopita, ikiwa na pointi moja zaidi ya Rubin Kazan na Barcelona huko Waukraine wakiwa nyuma zaidi.
Kiosi cha kocha Pep Guardiola kilikimbilia kumpata Zlatan Ibrahimovic na Lionel Messi amerejea katika ubora wake kwa ajili ya mchezo huo muhimu sana.
Mshambuliaji wa Argentina Messi alipata maumivu ya misuli Jumamosi wakati wakati timu yake ikitoka sare ya 1-1 na 1-1 katika mchezo wa La Liga huko Athletic Bilbao na Ibrahimovic aliukosa mchezo huo, kutokana na maumivu kama hayo.
Beki Eric Abidal na kiungo Yaya Toure wameambukizwa virusi vya homa ya mafua ya nguruwe lakioni Guardiola alikataa kupiga mayowe kuhusu matatizo yaliyomo katika kikosi chake.
"Endapo wachezaji hao hawatakuwepo...tutawatumia wachezaji wengine. Kamwe huwezi kutwaa taji ukiwa na wachezaji wawili au watatu tu, "alisema baada ya mchezo dhidi ya Bilbao.
Bayern Munich bado haijawahi kushinda mchezo wowote nyumbani katika Kundi A na , licha ya kesho Jumatano kuwa na kibarua chepesi kufuatia kupangwa kucheza na timu isiyo na uwezo sana ya Maccabi kesho, lakini imechelewa kuibuka.
Liverpool, ambayo inaweza kuzikosa fainaloi za msimu huu, tayari wamemkosa mshambuliaji wake muhimu Fernando Torres kwa ajili yamchezo wa leo Jumanne utakaopigwa Hungary katika Kundi E.
Timu ya kocha Rafael Benitez iko katika nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi lake ikiwa na pointi nne, tano nyuma ya Fiorentina.
Kushindwa kuibuka na ushindi katika mchezo huo kutaifanya Liverpool kuondolewa mapema endapo Fiorentina itaibuka na ushindi dhidi ya Lyon.
Vinara wa Kundi C Milan itafuzu hatua hiyo ya mtoano endapo itaifunga Olympique Marseille nyumbani kesho Jumatano.
Ushindi wa Milan pia utaiwezesha Real Madrid kufuzu mradi tu iwafunge mabingwa wa Uswisi FC Zurich, ambayo tayari iliteleza kwa kufungwa bao 12 baada ya kucheza mechi 12 na kufungwa 5-2 nyumbani dhidi ya klabu ya Hispania katika mechi za mapema.
Milan na Real - ambazo uwanja wao wa Bernabeu utaandaa fainali za Ligi ya Mabigwa wa Ulaya msimu huu, kila moja ina pointi saba, moja juu ya Marseille.

No comments:

Post a Comment