Tuesday, November 10, 2009

Keita 'out' siku 10


MADRID, Hispania
Kiungo wa Barcelona Seydou Keita ameshauriwa kupumzika kwa muda wa siku 10 baada ya kuumia goti.
Taarifa ya klabu hiyo--mabingwa wa vilabu barani Ulaya, ilisema jana kupitia tovuti yake (http://www.fcbarcelona.com/).
Keita aliumia wakati wa mechi ya ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Real Mallorca Jumamosi iliyopita, na anatarajia kuikosa mechi ya timu yake ya taifa ya Mali dhidi ya Ghana kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia.
Aidha, ataikosa mechi ya Barcelona kuwania Kombe la Mfalme Jumapili wiki hii dhidi ya Cultural Leonesa.

No comments:

Post a Comment