Tuesday, November 10, 2009

Ruvu Shooting, Simba uso kwa uso

Na Jacqueline Massano, Jijini

TIMU ya Ligi daraja la kwanza ya Ruvu Shooting inatarajia kushuka dimbani kesho kumenyana na Simba katika mechi ya kirafiki inayotarajia kufanyika kwenye uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Akizungumza na blog hii jana, Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Pwani, Hassan Othman 'Hassanoo' amesema mechi hiyo itakuwa ni moja ya maandalizi kwa timu hizo mbili.
Amesema Ruvu Shooting ambayo imetinga hatua ya tisa bora katika mechi ya ligi daraja ya kwanza inajiandaa na hatua hiyo ili iweze kufanikiwa kupanda daraja na kucheza ligi kuu ya Tanzania Bara.
Hassanoo ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya Simba, amesema mechi hiyo itatumiwa na wekundu hao wa Msimbazi kwa ajili ya kujiandaa na mechi yao dhidi ya Mtibwa Sugar.
Amesema kiingilio katika mechi hiyo kinatarajia kuwa sh. 5,000 kwa jukwaa kubwa, sh. 2,000 jukwaa la kijani na mzunguko sh. 1,000.

No comments:

Post a Comment