Tuesday, November 10, 2009

Munucho aomba radhi Angola

LUANDA, Angola
Mshambuliaji wa Manucho, ambeya amesimamishwa kwa kuchelewa kuripoti kwenye kambi ya timu ya taifa, ameomba msamaha, taarifa kutoka Luanda zimethibitisha jana.
"Naomba radhi kwa kocha, wachezaji wenzangu na wananchi wote kwa ujumla," alisema kupitia chombo cha habari kinachomilikiwa na serikali.
Angola, ambao ni wenyeji wa fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika kuanzia Januari 10-30, ina mechi za kimataifa za kirafiki dhidi ya Congo na Ghana.
Kocha Manuel Jose alisema wiki iliyopita kuwa Manucho, mchezaji wa zamani wa Manchester United, na sasa anacheza Real Valladolid ya Hispania, hatocheza mechi za timu ya taifa vinginevyo aombe radhi.

No comments:

Post a Comment