Thursday, November 26, 2009

Man Utd, Juventus chali

LONDON, England
BAYERN Munich, juzi ilijiweka katika nafasi nzuri ya kujinasua katika hatari ya kutolewa mapema katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya baada ya kuichapa Maccabi Haifa bao 1-0, huku wapinzani wao Juventus wakipokea kipigo kutoka kwa Girondins Bordeaux.
AC Milan wenyewe walikosa nafasi ya kujihakikishia kucheza hatua ya timu 16-bora baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Olympique Marseille, wakati Real Madrid ilipiga hatua moja mbele kuisogelea raundi ya pili kwa kuifunga FC Zurich 1-0 katika mechi ambayo winga Cristiano Ronaldo alikuwa dimbani baada ya muda mrefu wa kuwa majeruhi.
Manchester United, ambayo tayari ilishafuzu kwa raundi ya pili, ilijikuta ikiharibu rekodi yake ya kutofungwa mechi 23 nyumbani katika mashindano hayo baada ya kufungwa 1-0 kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford na timu ya Uturuki ya Besiktas.
Matokeo ya mechi za juzi hajaongeza idadi ya timu ambazo tayari zilizofuzu kwa hatua ya timu 16-bora, Girondins Bordeaux, Olympique Lyon, Arsenal, Manchester United, Chelsea, Porto, Fiorentina na Sevilla -- nafasi nane zilizobaki zitajazwa katika mechi za mwisho zitakazochezwa mwezi ujao.
Hatahivyo, bahati mbaya ya Bayern haikuwa mikononi mwao wakati mchezo huo ukianza, ambapo ilijua wazi kuwa ushindi kwa Juventus dhidi ya timu ambayo tayari ilishafuzu ya Bordeaux ungeiwezesha timu hiyo ya Italia kufuzu kwa raundi inayofuata.
Ikikabiliana na timu ambayo haijapata pointi hata moja au bao, Bayern ilifanya vitu vyake wakati Mcroatia Ivica Olic alipoipatia timu hiyo bao la ushindi katika dakika ya 62 alilofunga baada ya kuuwahi mpira uliorudi uwanjani na kuiwezesha timu hiyo kupata bao la kwanza nyumbani katika mechi tatu walizocheza katika kundi laoTimu ya Bordeaux inayofundishwa na Louis van Gaal iliibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Juventus huku mabao yakifungwa na Mbrazil Fernando na Mmorocco Marouane Chamakh katika kipindi cha pili.

No comments:

Post a Comment