Tuesday, December 1, 2009

Messi ashinda tuzo za Ballon D'or

PARIS, Ufaransa
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Barcelona na Argentina, Lionel Messi, ameshinda tuzo ya mwanasoka bora 2009 (Ballon D'Or), inayotolewana kila mwaka na jarida la michezo la Ufaransa, taarifa ya jarida hilo kupitia tovuti yake liliandika jana mjini Paris, nchini Ufaransa.
Messi, 22, anakuwa mchezaji wa kwanza wa Argentina kushindi tuzo hiyo, ambapo msimu iliopita alimaliza akiwa wa pili nyuma ya aliyekuwa mshindi Cristiano Ronaldo.
Taarifa za jarida hilo, zimesema kuwa Messi ameibuka mshindi wa tuzo hiyo baada ya kumshinda Cristiano Ronaldo aliyeshika nafasi ya pili kwa pointi 473 dhidi ya 233.
Messi, aliiwezesha mabingwa wa Hispania--Barcelona kutwaa taji la vilabu barani Ulaya msimu uliomalizika.
Mbali na kuiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa, pia aliweka rekodi nzuri ya kufunga mabao kwenye michuano hiyo baada ya kufanga mara tisa.
Moja ya bao hilo ni lile la mechi ya fainali dhidi ya Manchester United mjini Rome, Italia. Aliyeshika nafasi ya tatu na nne, ni wachezaji wenzake kwenye kikosi cha Barcelona, viungo Xavi (pointi 170) na Iniesta (pointi 149).
Mshambuliaji Samuel Eto'o, aliyeondoka Barcelona na kwenda kujiunga na Inter Milan msimu huu, alishika nafasi ya tano.
Mchezaji aliyeshika nafasi ya juu kwenye kinyang'anyoro hichi kutoka England ni Wayne Rooney aliyekuwa wa tisa.

No comments:

Post a Comment