Friday, November 13, 2009

Mrembo adakwa na 'unga'

LONDON,England
Mwanamitindo Kelly Askew, amakamatwa akiwa na dawa za kulevya aina ya cocaine zenye thamani ya paundi 627,000.
Dawa hizo zilikamatwa kwenye gari lake, polisi walisema. Wakati anakamatwa alikuwa kwenye gari lake aina ya Mercedes Benz lenye thamani ya paundi 12,000, sambamba na mpenzi wake John Clayton.
Walikamatwa karibu na barabara inayounganisha Bradford na West Yorks, mapema jana. Kabla ya kukamatwa walionekana wakikutana na mtu mmoja, taarifa zaidi zilidai.
Kisha polisi waliweka kizuizi na kuwakamata karibu na Bolton na kuwakuta wakiwa na kilo mbili za Cocaine ya kiwango cha juu. Askew, anayeishi Liverpool, alisema hajui lolote kuhusu mzigo huo, na kwamba mara nyingi amekuwa akimuendesha mpenzi wake kwa vile ana adhabu ya kutoendesha gari. Lakini polisi walisema simu ya kwenye gari ilionyesha kuwepo kwa mawasiliano kati ya Askew na Clayton, ambaye alikiri kumiliki mzigo huo.

No comments:

Post a Comment