Friday, November 13, 2009

Wachezaji Algeria washushiwa mvua za mawe

ALGIERS, Algeria
WACHEZAJI watatu wa timu ya taifa ya Nigeria, wamepata majeraha madogo baada ya basi walilopanda wakati wakiwasili mjini Cairo kushambuliwa kwa mawe na vijana, radio ya taifa ya Algeria ilitangaza jana.
Waziri wa mambo ya nje ya Algeria, amelaani tukio hilo ambalo limefanyika siku tatu kabla ya mechi muhimu itakayoamua ni timu gani kati ya Misri na Algeria itakayokwenda kucheza fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Afrika Kusini.
Taarifa zinasema kuwa, karibu vijana 200 walikuwa sehemu karibu na hotel ambayo timu hiyo ilipanga kufikia na kisha kurusha mawe kuelekea kwenye basi na kuvunja vioo kadhaa.
"Ni tukio baya la kujutia," alisema waziri wa Vijana na Michezo wa Algeria, Hachemi Djiar.
"Lakini pia basi lilipotoka uwanja wa ndege, vijana wengine pia walifanya shambulizi la mawe," aliongeza.
Hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa na viongozi wa Misri kuhusu tukio hilo.
Waziri anayehusika na dhamana ya michezo wa Algeria, alisema FIFA wana taarifa za tukio na walikuwa wakikutana kuamua nini cha kufanya.
Mechi ya Misri na Algeria inatarajia kuwa na upinzani mkali, kwani kama Algeria watashinda basi watakwenda kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza tangu waliposhiriki mara ya mwisho mwaka 1986.
Kushindwa kufuzu kwa Misri kwenye fainali za mwakani kutakuwa pigo kubwa kwao hasa ukizingatia kuwa wao ndio mabingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika.

No comments:

Post a Comment