Wednesday, December 2, 2009

Man Utd yaiadhibu Spurs

LONDON, England
Mchezaji Darron Gibson jana aliwawezesha mabingwa Manchester United kucheza hatua ya nne-bora ya Kombe Ligi kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tottenham Hotspur, matokeo ambayo yamezima ndoto za wapinzani wao kucheza hatua ya fainali ya michuano hiyo kwa mwaka wa tatu mfululizo.
United, waliowachapa kwa mikwaju ya penati Spurs msimu uliokwisha kwenye uwanja wa Wembley, watakumbana na Aston Villa katika mchezo wa nusu fainali baada ya wao nao kupata ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Portsmouth 4-2 kwenye uwanja wa Fratton Park.
'Matajiri' Manchester City watakutana na Arsenal, huku vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea ikisafiri kuifuata Blackburn Rovers katika mechi za robo fainali zitakazochezwa leo.
Kiungo wa kimataifa wa Ireland, Gibson alikuwa wa kwanza kupachika bao wavuni katika dakika ya 16, kabla ya kuongeza bao lingine katika dakika ya 22 kwa shuti kali la umbali wa mita 18. Kikosi cha vijana wa United kilicheza vizuri, lakini walikuwa Tottenham waliong'ara zaidi hasa kipindi cha kwanza wakisaka ushindi wa kwanza kwenye uwanja wa Old Trafford katika kipindi cha miaka 20.
Jermain Defoe kidogo afunge bao baada ya kumjaribu kipa wa United, Tomasz Kuszczak kwa shuti katika dakika ya saba tu, na alikuwa na nafasi nyingine nzuri ya kusawazisha makosa ya awali katika dakika ya 21 lakini jitihada zaje zilizuiwa na beki Nemanja Vidic

No comments:

Post a Comment