Wednesday, December 2, 2009

Yanga bado yamng'ang'ania Ambani

Jacqueline Massano, Jijini
PAMOJA na mshambuliaji Mkenya wa Yanga, Boniface Ambani kusisitiza hana mpango na timu hiyo, lakini uongozi wa klabu hiyo umezidi kudai kuwa ni mchezaji wao halali kutokana na kutompatia barua yoyote ya kusitisha mkataba wake.
Kauli ya Yanga, imekuja baada ya mshambuliaji huyo mrefu wa Kenya kusisitiza kutotambua kurejeshwa kwake kundini baada ya awali kuonekana 'kudhalilishwa' kwenye vyombo vya habari kwamba ametemwa kwa kushuka kwa kiwango chake cha uchezaji.
"Ni kweli awali tulikuwa na mpango wa kumuacha, na tulipanga kumpa barua ya kusitisha mkataba wake atakaporudi kutoka Kenya, lakini tumesitisha uamuzi wetu baada ya kuona hajapata timu ya kuchezea hadi sasa.
"Na sheria za Shirikisho la Soka nchini,TFF, ni kwamba kama klabu inataka kumuacha mchezaji mwenye mkataba ni lazima awe amepata timu kwanza," alisema Afisa Habari wa Yanga Luis Sendeu alipokuwa akizungumza na blog hii asubuhi ya leo
Sendeu alisema kinachotakiwa ni mchezaji huyo kuja nchini kwa ajili ya kujiunga na wenzake ambao wanaendelea na mazoezi na wala si kusikiliza maneno ya vyombo vya habari.
"Kama Ambani atakuwa anafanyakazi na vyombo vya habari atakuwa anafanya makosa, anachotakiwa ni kuwasikiliza viongozi wake, kwani sisi hatujampa barua ya kukatisha mkataba wake," alisema.
Alisema ikiwa mchezaji huyo ataamua kukatisha mkataba yeye mwenyewe atatakiwa kuilipa Yanga na wala si vinginevyo.
Sakata la Yanga na mchezaji huyo kwa sasa limeingiliwa na TFF, ambayo imethibitisha kuwa Ambani ni mchezaji halali wa Yanga kwa kuwa bado ana mkataba nayo.
PAMOJA na mshambuliaji Mkenya wa Yanga, Boniface Ambani kusisitiza hana mpango na timu hiyo, lakini uongozi wa klabu hiyo umezidi kudai kuwa ni mchezaji wao halali kutokana na kutompatia barua yoyote ya kusitisha mkataba wake.Kauli ya Yanga, imekuja baada ya mshambuliaji huyo mrefu wa Kenya kusisitiza kutotambua kurejeshwa kwake kundini baada ya awali kuonekana 'kudhalilishwa' kwenye vyombo vya habari kwamba ametemwa kwa kushuka kwa kiwango chake cha uchezaji."Ni kweli awali tulikuwa na mpango wa kumuacha, na tulipanga kumpa barua ya kusitisha mkataba wake kutoka Kenya, lakini tumesitisha uamuzi wetu baada ya kuona hajapata timu ya kuchezea hadi sasa."Na sheria za Shirikisho la Soka nchini,TFF, ni kwamba kama klabu inataka kumuacha mchezaji mwenye mkataba ni lazima awe amepata timu kwanza," alisema Afisa Habari wa Yanga Luis Sendeu alipokuwa anazungumza na Alasiri mapema leo.Sendeu alisema kinachotakiwa ni mchezaji huyo kuja nchini kwa ajili ya kujiunga na wenzake ambao wanaendelea na mazoezi na wala si kusikiliza maneno ya vyombo vya habari."Kama Ambani atakuwa anafanyakazi na vyombo vya habari atakuwa anafanya makosa, anachotakiwa ni kuwasikiliza viongozi wake, kwani sisi hatujampa barua ya kukatisha mkataba wake," alisema.Alisema ikiwa mchezaji huyo ataamua kukatisha mkataba yeye mwenyewe atatakiwa kuilipa Yanga na wala si vinginevyo.Sakata la Yanga na mchezaji huyo kwa sasa limeingiliwa na TFF, ambayo imethibitisha kuwa Ambani ni mchezaji halali wa Yanga kwa kuwa bado ana mkataba nayo.

No comments:

Post a Comment