Thursday, December 3, 2009

Nyoso, Makasi kuikosa Burundi


WACHEZAJI wa timu ya taifa 'Taifa Stars', Kigi Makasi na Juma Nyoso kesho hawatakuwepo kwenye kikosi cha timu yao kutokana na kupewa kadi nyekundu katika mechi tofauti ya michuano ya Kombe la Chalenji inayoendelea mjini Nairobi, Kenya.
Stars inatarajia kushuka dimbani kesho kumenyana na Burundi ili iweze kupata tiketi ya kucheza robo fainali ya michuano hiyo.
Nyoso alikuwa wa kwanza kulimwa kadi nyekundu wakati timu hiyo ilipokuwa inamenyana na Uganda na Stars kuchapwa bao 1-0, huku Makasi alilimwa kadi nyekundu wakati Stars ilipokuwa inacheza na Zanzibar Herous na kuibuka na ushindi wa bao 1-0.

No comments:

Post a Comment