Thursday, December 3, 2009

Papic akagua Kaunda

Na Jacqeline Massano
KOCHA mkuu wa mabingwa wa soka nchini, Yanga, Kostadin Kondic jana aliukagua Uwanja wa timu hiyo wa Kaunda uliopo makao makuu ya klabu hiyo ambao kwa sasa unaendelea na unaendelea na ularabati.
Afisa Habari wa mabingwa hao wa Jangwani, Loius Sendeu alisema Papic anataka uwanja huo ukarabatiwe haraka ili uweze kutumika kwa ajili ya mazoezi ya timu hiyo.
Anasema wakati wa kuukagua amegundua kuwa bado kuna mambo kadhaa hayajamaliziwa hivyo waliwataka wajenzi wa uwanja huo waharakishe ili umalizike kwa wakati.
"Kuna mambo madogo ambayo hayajamalizika, ila ukimalizika tu, timu itakuwa inautumia kwa ajili ya kufanya mazoezi ikiwa ni pamoja na kucheza mechi ndogondogo za kirafiki. Lakini wale wajenzi wamemuahidi kuwa utamalizika mapema," alisema
Wakati huo huo, Yanga imethibitisha kushiriki kwenye mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayotarajia kuanza kufanyika Jumamosi mjini Zanzibar.
Mashindano hayo ambayo fainali zake zinatarajia kufanyika Januari 12 mwakani, yanatarajia kuzishirikisha timu za Mtibwa Sugar, Yanga, Simba, Miembeni, Mafunzo, Malindi na Zanzibar Ocean View.

No comments:

Post a Comment