Friday, December 4, 2009

Ratiba Kombe la Dunia kupangwa leo

CAPE TOWN, Afrika Kusini
AFRIKA Kusini imesema vitendo vyovyote vya kihalifu havitavumilika wakati wa fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini humo, na kwa sababu hiyo imejiandaa vizuri kiusalama ambapo vifaa vya kisasa vya ulinzi vitatumika.
Nchi hiyo yenye rekodi mbaya ya matukio ya kihalifu lakini ikiwa nje ya ukanda wa kivita, imesema itaongeza idadi kubwa ya polisi wakati wa fainali hizo zitakazodumu kwa muda wa mwezi mmoja.
Tangazo hilo limekuja huku maafisa na mashabiki wakionyesha mashaka kutokana na kuendelea kwa vitendo vya uhalifu.
"Kwa sasa, wakati tunasubiri kupangwa kwa ratiba ya fainali za mwaka 2010, na zikiwa zimesalia siku kama 187 kabla ya kuanza kwa michuano, timejiandaa vya kutosha kwa asilimia 100," alisema Waziri wa Polisi, Nathi Mthethwa.
Ratiba ya michuano hiyo itakayozishirikisha timu 32, inatarajia kutolewa jioni ya leo, ambapo askari 1,000 wakashiriki katika kulinda usalama.
Mwanasoka wa kimataifa wa England, David Beckham anatarajia kushiriki katika hafla hiyo.
Mthethwa alisema polisi watasambazwa kwenye hotel, huku wengine wakiwa na nguo za kiraia, huku wengine wakifanya kazi kwa siri zaidi ili kupambana na vitendo vyovyote vya kihalifu.
Afrika Kusini iko katika mkakati mkali wa kupambana na matukio ya kihalifu wakati wa fainali za mwakani, ambapo serikali ya nchi hiyo imeuhakikishia ulimwengu kuwa usalama utakuwepo kwa asilimia 100 ili wageni wapatao 450,000 wakataokuja kushuhudia michuano hiiyo hawapati usumbufu.
Septemba mwaka huu, Mthethwa alitoa taarifa inayoonyesha kupungua kwa vitendo vya kihalifu kati ya Aprili 2008 to Machi 2009.

No comments:

Post a Comment